Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa an
Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Ndugu Jumanne Sagini, amesema kuwa
wanafunzi wote waliofaulu vizuri masomo ya sayansi na wanapenda kusoma
masomo hayo lakini walipangiwa masomo ya sanaa kutokana na kukosa
nafasi, wanayo fursa ya kubadilisha kupitia kwa wakuu wao wa shule; na
endapo kwenye shule walizopangwa hakuna tahasusi za masomo ya Sayansi
wanaweza kuwasilisha maombi yao kwa Maafisa elimu Mikoa ambapo shule
hizo zipo, kupitia kwa wakuu wa shule walizopangiwa, ili waweze
kubadilishiwa tahasusi za sayansi kwenye shule zilizopo kwenye Mikoa
husika.
|
|
Ngugu Jumanne Sagini aliyasema hayo katika mkutana na
waandishi wa habari uliofanyika tarehe Julai 22, 2014 katika Ofisi za
OWM-TAMISEMI, Dar es Salaam.
|
|
“Tumetoa maagizo kwa wakuu wa shule na maofisa Elimu
wa Wilaya na Mikoa kuhakikisha wanafunzi waliofaulu masomo ya sayansi na
kupangiwa sanaa wanabadilishiwa iwapo watataka.” Alisema ndugu Jumanne
Sagini.
|
|
Aidha ndugu jumanne Sagini alisema kuwa Serikali kwa
kutambua umuhimu wa masomo ya sayansi na mwitikio chanya uliopo sasa kwa
wanafunzi kusoma masomo hayo, imeendelea kuimarisha miundombinu ya
shule kwa kutoa fedha za ujenzi, ukamilishaji na ukarabati. Pia,
Serikali inatarajia kufanya uchaguzi wa awamu ya pili kwa wanafunzi
waliobaki kutokana na ufinyu wa nafasi za shule za kidato cha tano,
baada ya kubaini uwepo wa nafasi hizo; na inatarajiwa kwamba baadhi ya
wanafunzi wenye sifa watachaguliwa kwenda kusomea ualimu na vyuo vingine
vya ufundi.
|
|
Katika matokeo ya mtihani kwa mwaka 2014, inaonyesha
kuwa jumla ya wanafunzi 22,685 kati yao Wasichana 7,859 na Wavulana
14,826 wamechaguliwa kusoma tahasusi za sayansi ikilinganishwa na idadi
ya wanafunzi 18,746 kati yao Wasichana 5,038 na Wavulana 13,708 kwa
mwaka 2013. Aidha tofauti na miaka mingine iliyopita, Ufaulu wa
watahiniwa wa shule kwa mwaka 2013 katika madaraja ya I -III umeongezeka
kutoka watahiniwa 35,357 mwaka 2012 hadi 71,527 mwaka huu. Ufaulu huu
ni zaidi ya asilimia mia moja ya watahiniwa waliokuwa na sifa za
kuendelea na masomo ya kidato cha tano mwaka 2013.
|
|
“Natoa pongezi nyingi kwa walimu,
wanafunzi,wazazi/walezi na wadau wote wa elimu kwa juhudi walizozifanya
kuwezesha ufaulu katika masomo ya sayansi kuongezeka kwa kiasi cha
kuridhisha.” Alisema ndugu Jumanne Sagini.
Pia ndugu Jumanne Sagini alieleza kuwa matokeo
haliyotangazwa mwaka huu 2014 yanakaribia sana malengo ambayo Serikali
imejiwekea kupitia Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (yaani Big Results
Now-BRN) ambapo serikali ilijiwekea lengo la kuhakikisha wanafunzi
wanafaulu kwa asilimia 60 mwaka 2013. Matokeo halisi yanaonyesha kuwa
ufaulu umepanda kutoka asilimia 43 mwaka 2012 hadi asilimia 58.25 mwaka
2013.
|
|
Wakati huohuo shule zote zilizofanya vibaya katika
matokeo ya Kidato cha Sita mwaka huu 2014, ambapo mazingira na nafasi
yake iliruhusu kufanya vizuri, zimeamriwa kujieleza sababu za kufanya
vibaya.
|
|
Ndugu Jumanne Sagini alisema kuwa Makatibu Tawala
Mkoa wameagizwa kutoa maelezo na kufanya utafiti ndani ya mwezi kubaini
sababu ya shule hizo kufanya vibaya ili hatua stahiki zichukuliwe, hali
hiyo isijirudie.
|
|
“Tumetaka maelezo kutoka kwa Makatibu Tawala Mkoa; kwa
nini shule zimefanya vibaya. Matokeo ya hovyo kama haya ni jambo
lisiloweza kueleweka; na wasimamizi wa elimu nimewaambia halikubaliki.”
Alsema ndugu Sagini.
|
|
Aidha ndugu Sagini aliendelea kusema “Shule kongwe
kama Tambaza na Iyunga, zinazopewa fedha na Serikali, zina walimu wa
kutosha, zina maabara, nyumba za walimu lakini bado matokeo yanakuwa ya
hovyo, tunataka kujua sababu”.
|
|
Ndugu Sagini aliendelea kusema: “Sisi wenyewe
imetuudhi, imetuhuzunisha na kwa kweli haikuwa matarajio ya Serikali kwa
shule kongwe kuwa na matokeo mabaya”.
|
|
Hata hivyo alisema kuwa anazo taarifa za kuwepo kwa
vikao vya kushughulikia matokeo mabaya katika shule ya sekondari Tambaza
iliyopo jijini Dar es Salaam.
|
|
Aidha aliainisha kuwa tatizo lililochangia baadhi ya
shule kufanya vibaya ni kukosa usimamizi makini, hivyo aliwataka wakuu
wa shule kutimiza wajibu wao.
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
0 comments:
Post a Comment