Tuesday 29 May 2018

JKT : MAJINA YA WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA JKT MUJIBU WA SHERIA 2018

 


 TAARIFA KWA UMMA

Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), limefanya uteuzi wa wanafunzi waliohitimu elimu ya sekondari kidato cha sita kutoka shule zote za Tanzania Bara kwa mwaka 2018, kuhudhuria mafunzo ya JKT kwa mujibu wa Sheria.

Sanjari na uteuzi huo, JKT limewapangia Makambi ya JKT watakayokwenda kupatiwa mafunzo kwa muda wa miezi mitatu na wanatakiwa kuripoti makambini kuanzia tarehe 01-10 June 2018.

Wahitimu hao, wamepangiwa katika Kambi za JKT Rwamkoma – Mara, JKT Msange – Tabora, JKT Ruvu – Pwani, JKT Makutupora – Dodoma, JKT Mafinga – Iringa, JKT Mlale – Ruvuma, JKT Mgambo na JKT Maramba – Tanga, JKT Makuyuni – Arusha, JKT Bulombora, JKT Kanembwa, Nachingwea- Lindi na JKT Mtabila – Kigoma.

Aidha, wahitimu wenye ulemavu wa kuonekana kwa macho (physical disabilities) wanatakiwa kuripoti kambi ya Ruvu JKT iliyopo mkoani Pwani ambayo ina miundombinu ya kuhudumia wa jamii hiyo.

Vijana watakaochaguliwa watatakiwa kujigharamia nauli za kwenda na kurudi kwenye makambi ya JKT waliyopangiwa wakiwa na vifaa vifuatavyo:

  1. Bukta ya rangi ya Dark blue yenye mpira kiunoni (lastic), iliyo na mfuko mmoja nyuma, urefu unaoishia magotini isiyo na zipu. Aidha bukta za wanawake zinatakiwa kuwa na lastic magotini.
  2. Raba za michezo zenye rangi ya kijani.
  3. Shuka mbili za kulalia zenye rangi ya blue bahari.
  4. Soksi ndefu za rangi nyeusi.
  5. Nguo za kuzuia baridi kwa waliopangwa kwenye mikoa yenye baridi.
  6. Track Suit ya rangi ya kijana au bluu

Mkuu wa JKT anawakaribisha vijana wote walioteuliwa ili waweze kujiunga na vijana wenzao katika kujifunza Uzalendo, Umoja wa Kitaifa, stadi za kazi, stadi za maisha na Utayari wa kulijenga na kulitumikia Taifa letu.

Orodha kamili ya majina ya vijana na makambi ya JKT waliyopangiwa vinapatikana kwenye tovuti ya JKT ambayo ni www.jkt.go.tz



 BOFYA JINA LA KIKOSI HAPO CHINI  KUANGALIA MAJINA YA VIJANA WA MUJIBU WA SHERIA AWAMU YA KWANZA  2018 

  BULOMBORA JKT-KIGOMA                    RWAMKOMA JKT -MARA                  MSANGE JKT-TABORA

  KANEMBWA JKT-KIGOMA                      MTABILA-KIGOMA                            RUVU JKT-PWANI

  MAKUTUPORA JKT- DODOMA                MGAMBO JKT-TANGA                      MARAMBA JKT- TANGA

  MAFINGA JKT- IRINGA                          NACHINGWEA-LINDI                       MLALE JKT -RUVUMA

  MAKUYUNI-ARUSHA

Share:

JKT : Tarehe ya mwisho kuripoti makambini Vijana waliohitimu elimu ya kidato cha sita mwezi Mei 2017



 TAARIFA KWA UMMA

Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), linautangazia Umma mabadiliko ya tarehe ya mwisho kuripoti makambini Vijana waliohitimu elimu ya kidato cha sita mwezi Mei 2017 na kuchaguliwa kujiunga na Mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa Sheria mwaka 2017.

Tarehe ya mwisho kwa vijana hao kuripoti makambini imesogezwa mbele hadi tarehe 09 June 2017.

Mkuu wa JKT anawakaribisha vijana wote waliochaguliwa ili waweze kujiunga na vijana wenzao katika kujifunza uzalendo, umoja wa kitaifa, stadi za kazi, stadi za maisha na utayari wa kulijenga na kulitumikia Taifa letu. Atakayesikia tangazo hili amtaarifu na mwenzie.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Habari na Uhusiano,
Makao Makuu ya JKT,
Tarehe 30 Mei 2017

Share:

Friday 25 May 2018

NACTE : EMPLOYMENT OPPORTUNITY MAY18, 2018

NATIONAL COUNCIL FOR TECHNICAL EDUCATION
EMPLOYMENT OPPORTUNITY
National Council for Technical Education (NACTE) was established by the National Council for Technical Education Act, Cap. 129 (No. 9 of 1997). The Council is a body corporate with a legal mandate of coordinating provision of technical education and training. The Council is also mandated to establish an efficient national qualifications system that will ensure that products from technical institutions are of high quality and respond to changing needs as well as technological innovations in the world. The Council is hereby seeking to engage a well self-motivated individual who is capable to work independently to fill in the following vacant position:
1.0 JOB DETAILS
  1. Job Title: Executive Secretary
  2. Appointment: National Council for Technical Education
  3. Responsible to: NACTE Council
2.0 JOB SUMMARY
The Executive Secretary (ES) is the Chief Executive Officer of the Secretariat. The ES is responsible to the Council for implementing the policies of the Council including planning, coordinating and controlling all functions and activities within the framework and instructions laid down by the Council in accordance with the Act. The ES is further responsible to the Council for the general direction, leadership, administration and supervision of all Council's staff and operations. The ES is expected to manage and develop NACTE to an effective, efficient and credible institution to meet its functions and objectives as stipulated in the establishing Act, Cap, 129 (No. 9 of 1997) and any subsequent amendments.
3.0 MINIMUM QUALIFICATIONS AND EXPERIENCE
A potential candidate for this post should have the following qualifications and experience:
  1. Holder of a Doctorate Degree (PhD) in one of the following areas:
    1. Science and Allied Technologies,
    2. Business, Management and Planning,
    3. Health and Allied Sciences,
    4. Teaching and Learning Facilitation,
    5. Any other related academic qualification.
  2. Must have a minimum of ten (10) years working experience at senior managerial level in education management at tertiary education level in accredited technical and vocational training institution(s).
  3. Must have ability to solicit funds from other sources apart from the Government subvention.
4.0 MAIN DUTIES AND RESPONSIBILITIES
The main duties and responsibilities of the Executive Secretary shall include to:
  1. Develop policies for approval by the Council.
  2. Ensure the implementation of policies and procedures approved by the Council.
  3. Ensure effective and efficient liaison with other relevant bodies with a view of providing strategic advice on the development of technical education and training.
  4. Organise and service meetings of the Subject Boards and the Council,Serve as Accounting Officer of the Council and accountable for the resources entrusted to it.
  5. Direct the operations of the Secretariat.
  6. Develop Strategic Plans, Annual Plans and Budget taking into account the Council's Vision and Mission with a view to making NACTE effective and efficient.
  7. Ensure that the Council’s initiatives are consistent with Government policies,
  8. Submit to the Council at the end of every three months a reports on:
    1. Its performance and other related information.
    2. The operations of the Council.
    3. Such other information as the Council may direct.
  9. Supervise, coach and mentor subordinates to ensure their performance is aligned with the Council’s goals and objectives.
  10. Promote awareness and an understanding of the Council’s mission, objectives,
  11. policies and programmes among all stakeholders.
5.0 REMUNERATION TERMS AND CONDITIONS
Successful candidate will be paid according to NACTE salary scale and will hold the office for a period of three (3) years renewable upon satisfactory performance review.

6.0 MODE OF APPLICATION
  1. Applicants, who meet the stated requirements for the advertised post and would like to serve the Tanzanian Public Service through NACTE, should send their applications to: The Chairman, Search Team for Executive Secretary NACTE, Ardhi University, University Road, and P.O. Box 35176 Dar es Salaam.
  2. Signed application letters must be accompanied by:
    1. Proof of Tanzanian citizenship (affidavits will not be accepted).
    2. Applicant’s current CV and two passport size photographs in colour.
    3. Photocopies of official academic transcripts and professional certificates.
    4. Names and full contact addresses and daytime telephone numbers of three referees.
  3. All applications must be posted by registered mail preferably EMS.
  4. Applications should reach the addressee latest by the close of business on 4th June 2018.
  5. The title of the position applied for must be marked on the envelope to make the application valid.
NOTE: Only short-listed candidates who meet the above criteria will be contacted and those who will not hear from the Chairman of the Search Team should consider themselves unsuccessful.
Share:

HESLB : HESLB YAANZA KUPOKEA MAOMBI YA MIKOPO 2018/2019

  Image result for WANAPORTAL HESLB

HESLB YAANZA KUPOKEA MAOMBI YA MIKOPO 2018/2019

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) leo imetangaza kuanza kupokea maombi ya mikopo ya elimu ya juu kwa muda wa miezi miwili na kusisitiza kuwa maombi yote yatapokelewa kwa njia ya mtandao.

Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru (pichani) amesema leo jijini Dar es salaam  wakatik akifungua rasmi kuwa mtandao wa kuwasilisha maombi ya mkopo (www.olas.heslb.go.tz) utakuwa wazi kuanzia Mei 10, 2018 hadi Julai 15, 2018 ili kuwapa fursa wanafunzi wahitaji kuwasilisha maombi yao.

“Mwaka jana tulitoa mwezi mmoja, mwaka huu tumetoa muda zaidi ili kuwawezesha kusoma mwongozo kwa makini na kuzingatia maelekezo tunayoyatoa,” amesema Bw. Badru katika mkutano na wanahabari ambapo pia alizungumzia mambo muhimu yaliyomo kwenye mwongozo unaojumuisha sifa na taratibu za utoaji mikopo kwa mwaka 2018/2019. Mwongozo huo unapatikana katika lugha za Kiswahili na Kiingereza kwenye tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz)

Mambo muhimu yaliyomo kwenye Mwongozo

Mkurugenzi Mtendaji amesema kuwa katika utoaji mikopo kwa mwaka 2018/2019, kipaumbele kitatolewa kwa watanzania wahitaji wanaosoma kozi zenye uhitaji mkubwa zaidi kitaifa kama walimu wa masomo ya sayansi na hisabati; na sayansi ya afya ya binadamu.

“Tutatoa kipaumbele pia kwa waombaji mikopo watakaodahiliwa katika kozi zinazohitajika kuchochea ukuaji wa uchumi wa viwanda kama uhandisi wa aina zote; kozi za sayansi za kilimo na wanyama na kozi zinazohusiana na gesi na nishati,” amesema Bw. Badru katika mkutano huo uliohudhuriwa na wawakilishi wa wadau wa HESLB kama Shirikisho la Serikali za Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu (TAHLISO); Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) na Shirika la Posta (TPC).

Aidha, ameongeza kuwa watanzania wahitaji ambao ni yatima na wana nakala za vyeti vya vifo vilivyothibitishwa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) nao watapewa kipaumbele bila kujali kozi wanazosoma. Wengine watakaopewa kipaumbele ni waombaji wenye ulemavu uliothibitishwa na Mganga wa Mkoa au Wilaya na waombaji mikopo ambao walifadhiliwa katika masomo yao ya stashahada (diploma) au sekondari na wana barua za uthibitisho kutoka taasisi zilizowafadhili.

Bajeti na idadi ya watakaopata mikopo kwa 2018/2019

Kuhusu malengo ya utoaji mikopo kwa mwaka wa masomo 2018/2019, Bw. Badru amesema Bodi imepanga kutoa mikopo kwa jumla ya wanafunzi wapya 40,000 na wanaoendelea zaidi ya 80,000. Kati yao, wanawake watakuwa asilimia 35 (14,000) na wanaume asilimia 65 (26,000). Bajeti ya fedha za mikopo kwa mwaka 2018/2019 ni TZs 427 bilioni.

Maboresho yanayoendelea

Kuhusu uboreshaji wa mifumo ya TEHAMA, Bw. Badru amesema Bodi ya Mikopo kwa kushirikiana na Kitengo cha Kompyuta cha Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UCC) wanaendelea na maboresho makubwa ili kuifanya mifumo ya utoaji na urejeshaji mikopo kuwa rafiki zaidi kwa wateja. Kazi hiyo inatarajiwa kukamilika mwezi Agosti mwaka huu.

“Kwa mfano, mfumo wa kuwasilisha maombi sasa umeboreshwa na kuwa rafiki zaidi kwa kuwa unamwongoza mwombaji katika kila hatua – na hatoweza kwenda hatua inayofuata kabla ya kukamilisha hatua ya awali,” amesema Bw. Badru.

Aidha, kwa mara ya kwanza, Bodi imetoa mwongozo wake wa uombaji mikopo katika lugha ya Kiswahili pamoja na kitabu chenye maswali na majibu 21 kuhusu sifa na utaratibu (hatua kwa hatua) wa kuwasilisha maombi ya mikopo. Kitabu na mwongozo vinapatikana katika tovuti ya Bodi na vitasambazwa kwa wadau kuanzia wiki ijayo ambapo maafisa wa Bodi watatembelea shule na waombaji nchini kote.

Maoni ya TAHLISO

Akiongea katika mkutano huo, Meneja Usajili wa RITA Bi. Patricia Mpuya amewahakikishia waombaji wa mikopo kuwa vyeti vya vifo na kuzaliwa ambavyo vitawasilishwa kwa taasisi hiyo kuwa vitahakikiwa ndani ya siku tatu.

“Tunawakumbusha kuhakikisha wanaleta maombi haraka badala ya kusubiri ‘deadline’ (muda wa mwisho) na sisi tumejipanga wanapata majibu ya uhakiki ndani ya siku tatu tangu tuyapokee,” amesema Bi. Mpuya.   

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Shirika Posta (TPC) Bw. Hassan Mwangombe, ambao watapokea na kusafirisha kwenda HESLB fomu za maombi ya mikopo, amesema wamejipanga kutoa huduma za elimu kwa waombaji na intaneti katika vituo vyao zaidi ya 180 nchini. Aidha, wameandaa bahasha maalum ambayo mwombaji mkopo atajaza taarifa zake muhimu ili kurahisisha uwasilishaji wa maombi hayo kwa HESLB.

Mwenyekiti wa TAHLISO Bw. George Mnali amezitaka RITA na TPC kuhakikisha wanatekeleza mipango yao ya kuwahudumia waombaji mikopo kama walivyoahidi na kuongeza TAHLISO itatumia muda wa miezi miwili kuwaelimisha wanafunzi wasio na mikopo lakini wana sifa kuomba na kufuata maelekezo ya Bodi.

Wito

Bodi imewataka waombaji mikopo kuzingatia maelekezo yaliyotolewa na wale ambao wana uwezo wa kugharamia elimu ya juu kutoomba mkopo ili kutoa fursa kwa wahitaji halisi wengi zaidi kuomba na kupata mikopo.

HESLB ilianza kazi rasmi mwaka 2005 ili, pamoja na majukumu mengine, kutoa mikopo ya elimu ya juu kwa watanzania wahitaji na wenye sifa na kukusanya mikopo iliyoiva ambayo ilitolewa na Serikali tangu mwaka 1994/1995.

Imetolewa na:

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu

DAR ES SALAAM

Alhamisi, Mei 10, 2018
Share:

HESLB: HESLB KUANZA KUPOKEA MAOMBI YA MIKOPO MEI 2018

Image result for WANAPORTAL HESLB

HESLB KUANZA KUPOKEA MAOMBI YA MIKOPO MWEZI HUU

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inapenda kuwataarifu wananchi kuwa inatarajia kuanza kupokea maombi ya mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2018/2019 kuanzia wiki ya kwanza ya mwezi Mei, 2018 baada ya kukamilishwa kwa maboresho makubwa ya mfumo wa uombaji kwa njia ya mtandao.
Maboresho ya mfumo wa maombi
Mkurugenzi MtendajiMkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru amesema katika taarifa yake ya Aprili 17, 2018 kuwa maombi yote yatapokelewa kwa njia ya mtandao (www.olas.heslb.go.tz) ambao umefanyiwa maboresho na Kituo cha Kompyuta cha Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UCC-UDSM).

Aidha, Bw. Badru amesema dirisha hilo litafunguliwa sambamba na kutangazwa kwa mwongozo wa kina utakaotoa utaratibu wa kuwasilisha maombi, tarehe ya mwisho ya kuwasilisha maombi, sifa na vigezo vitakavyotumika katika kuchambua na kutoa mikopo kwa mwaka ujao wa masomo unaotarajiwa kuanza mwezi Oktoba, 2018.

“Tunawasihi wale wote wanaotarajia kuomba mkopo wa elimu ya juu kusoma kwa makini mwongozo tutakaoutoa kwa vyombo vya habari na tovuti mwanzoni mwa mwezi Mei, 2018 na kuuzingatia,” amesema Bw. Badru.

Bw. Badru amefafanua kuwa wito wa Bodi ya Mikopo umetolewa kutokana na uzoefu wa miaka iliyopita ambapo waombaji wa mikopo waliwasilisha maombi yao bila kuzingatia mwongozo uliotolewa na kusababisha baadhi ya wanafunzi kukosa mikopo.

“Mwaka jana, kwa mfano, zaidi ya waombaji 10,027 kati ya waombaji zaidi ya 61,000 hawakuambatisha nyaraka muhimu kama vyeti vya kuzaliwa au hata vile vya vifo vilivyothibitishwa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) kama tulivyoelekeza,” amesema.

Nyaraka muhimu zinazohitajika
Nyaraka nyingine muhimu ambazo waombaji mikopo wanapaswa kuziandaa ni pamoja na nakala za vyeti vya kitaaluma za kidato cha nne, sita na stashahada ambazo zimethibitishwa na Kamishna wa Viapo yaani Wakili au Hakimu.

Aidha, wanafunzi waombaji wenye ulemavu au wenye wazazi wenye ulemavu wanapaswa kuwa na barua zinazothibitisha ulemavu huo kutoka kwa Mganga Mkuu wa Mkoa, Wilaya au Kituo cha Afya cha Serikali;

Bw. Badru ameongeza kuwa wanafunzi ambao walifadhiliwa katika masomo yao ya Sekondari au Stashahada (Diploma) wawe na barua za uthibitisho wa udhamini huo kutoka katika taasisi zilizogharamia masomo yao.

Maafisa wa HESLB kutoa elimu mikoani
Katika hatua nyingine, Bw. Badru amesema mwaka huu maafisa wa Bodi ya Mikopo watatembelea mikoa mbalimbali ili kukutana na waombaji mikopo kwa lengo la kuwaelimisha kuhusu taratibu sahihi za kuwasilisha maombi yao ya mikopo kwa njia ya mtandao. Ratiba na maeneo itakapofanyia mikutano hiyo itatangazwa mwanzoni mwa mwezi Mei, 2018. 

HESLB ilianza kazi rasmi mwaka 2005 ili, pamoja na majukumu mengine, kutoa mikopo ya elimu ya juu kwa watanzania wahitaji na wenye sifa na kukusanya mikopo iliyoiva ambayo ilitolewa na Serikali tangu mwaka 1994/1995.

Imetolewa na:
Abdul-Razaq Badru
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
DAR ES SALAAM
Kwa ufafanuzi: +255 (0) 757 500800
Share:

Monday 7 May 2018

HESLB : IMPORTANT NOTICE TO ALL LOAN APPLICANTS FOR 2018/2019

 Higher Education Students' Loans Board

  Image result for HEsLB wanaportal

IMPORTANT NOTICE TO ALL LOAN APPLICANTS FOR 2018/2019

This is to inform all expected loan applicants (new and continuing students) for 2018/2019 that our online loan application window will be open from Thursday, May 10th, 2018 to Sunday, July 15th, 2018.
 For now, expected loan applicants are requested to familiarize themselves with the ‘Guidelines and Criteria for Issuance of Loans for 2018/2019 Academic Year.’
 Click here to view the Guidelines and Criteria for Issuance of loans for 2018/2019

 Issued by the Higher Education Students’ Loans Board
Monday, May 7th, 2018

Share: