Wednesday 12 June 2019

JKT :VIFAA AMBAVYO VIJANA WA MUJIBU WA SHERIA 2019 WANATAKIWA KURIPOTI NAVYO MAKAMBINI


JESHI LA KUJENGA TAIFA

                                                                                                                                       




TAARIFA KWA UMMA

Vijana waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria mwaka 2019 wanatakiwa kuripoti makambini na vifaa vifuatavyo:-
  1. Flana ya rangi ya kijani kibichi yenye kora ya duara (Dark Green T-shirt with round collar).
  2. Bukta ya rangi ya ‘Dark Blue’ yenye mpira kiunoni (lastic), iliyo na mfuko mmoja nyuma, urefu unaoishia magotini, isiyo na zipu.
  3. Raba za michezo zenye rangi kijani au blue.
  4. Shuka mbili za kulalia zenye rangi ya blue bahari.
  5. Soksi ndefu za rangi nyeusi.
  6. Nguo za kuzuia baridi kwa waliopangiwa mikoa yenye baridi.
  7. Track suit ya rangi ya kijani au blue
  8. Nauli ya kwenda makambini na kurudi nyumbani.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Habari na Uhusiano,
Makao Makuu ya JKT,
Tarehe 24 Mei 2019.
Share:

1 comment: