BARAZALAMITIHANI LA TANZANIA
MWONGOZO WAMATUMIZI YA VIWANGO VYA UFAULU
NA UTARATIBU WA KUTUNUKU MATOKEO YA KIDATO
CHA NNE NA KIDATO CHA SITA
1.0 UTANGULIZI
Ipo mifumo anuwai inayotumiwa na Nchi mbalimbali duniani katika kupanga viwango vya ufaulu kwa ajili ya kutunuku vyeti kwa watahiniwa waliofanya mitihani ya Taifa. Hata hivyo, mfumo wenye kutumia Viwango vya Ufaulu vinavyobadilika (Flexible Grade Ranges) na Viwango vya
Ufaulu visivyobadilika (Fixed Grade Ranges) hutumika zaidi ikilinganishwa na mifumo mingine. Upangaji wa viwango katika Nchi zinazotumia mfumo wa viwango vinavyobadilika hutegemea jinsi watahiniwa walivyofaulu somo husika. Katika mfumo huo, viwango vya ufaulu huweza kutofautiana baina ya somo na somo na kati ya mwaka mmoja na mwingine kwa sababu kiwango cha ufaulu hutofautiana baina ya somo moja na jingine. Aidha, kwa nchi zinazotumia mfumo wa viwango vya ufaulu visivyobadilika (Fixed Grade Ranges), viwango vya ufaulu vinavyofanana hupangwa ili vitumike kama kipimo cha ufaulu kwa masomo yote kwa kila mwaka.
Tanzania ilikuwa ikitumia mfumo wa viwango vya ufaulu vinavyobadilika (Flexible Grade Ranges) kuanzia mwaka 1973 hadi 2011. Hata hivyo, kuanzia Mtihani wa Kidato cha Nne 2012, Baraza la Mitihani la Tanzanialiliamua kuanza kutumia mfumo wa Viwango vya Ufaulu visivyobadilika
(Fixed Grade Ranges) kwa madhumuni ya kuwawezesha wadau kujua viwango vya ufaulu vinavyotumika katika kutunuku matokeo ya Mitihani ya Taifa.
Baraza la Mitihani limeandaa Mwongozo huu ili kuwawezesha wadau mbalimbali wa elimu kufahamu viwango vya ufaulu vilivyoidhinishwa kutumika katika Mitihani ya Kidato cha Nne na Kidato cha Sita. Aidha, mwongozo huu umebainisha utaratibu unaotumika katika kutunuku
matokeo ya mitihani hiyo kwa lengo la kuwawezesha wadau wa elimu kuongeza chachu katika ufundishaji na ujifunzaji ili kufikia viwango vya juu vya ufaulu vilivyobainishwa na Baraza la Mitihani la Tanzania.
Sehemu ya pili ya Mwongozo huu inafafanua malengo ya Mitihani ya Kidato cha Nne na Kidato cha Sita. Aidha, sehemu ya tatu inafafanua utaratibu wa kutunuku viwango vya ufaulu na sehemu ya nne ni hitimisho.
Ufaulu visivyobadilika (Fixed Grade Ranges) hutumika zaidi ikilinganishwa na mifumo mingine. Upangaji wa viwango katika Nchi zinazotumia mfumo wa viwango vinavyobadilika hutegemea jinsi watahiniwa walivyofaulu somo husika. Katika mfumo huo, viwango vya ufaulu huweza kutofautiana baina ya somo na somo na kati ya mwaka mmoja na mwingine kwa sababu kiwango cha ufaulu hutofautiana baina ya somo moja na jingine. Aidha, kwa nchi zinazotumia mfumo wa viwango vya ufaulu visivyobadilika (Fixed Grade Ranges), viwango vya ufaulu vinavyofanana hupangwa ili vitumike kama kipimo cha ufaulu kwa masomo yote kwa kila mwaka.
Tanzania ilikuwa ikitumia mfumo wa viwango vya ufaulu vinavyobadilika (Flexible Grade Ranges) kuanzia mwaka 1973 hadi 2011. Hata hivyo, kuanzia Mtihani wa Kidato cha Nne 2012, Baraza la Mitihani la Tanzanialiliamua kuanza kutumia mfumo wa Viwango vya Ufaulu visivyobadilika
(Fixed Grade Ranges) kwa madhumuni ya kuwawezesha wadau kujua viwango vya ufaulu vinavyotumika katika kutunuku matokeo ya Mitihani ya Taifa.
Baraza la Mitihani limeandaa Mwongozo huu ili kuwawezesha wadau mbalimbali wa elimu kufahamu viwango vya ufaulu vilivyoidhinishwa kutumika katika Mitihani ya Kidato cha Nne na Kidato cha Sita. Aidha, mwongozo huu umebainisha utaratibu unaotumika katika kutunuku
matokeo ya mitihani hiyo kwa lengo la kuwawezesha wadau wa elimu kuongeza chachu katika ufundishaji na ujifunzaji ili kufikia viwango vya juu vya ufaulu vilivyobainishwa na Baraza la Mitihani la Tanzania.
Sehemu ya pili ya Mwongozo huu inafafanua malengo ya Mitihani ya Kidato cha Nne na Kidato cha Sita. Aidha, sehemu ya tatu inafafanua utaratibu wa kutunuku viwango vya ufaulu na sehemu ya nne ni hitimisho.
2.0 MALENGO YA MITIHANI YA KIDATO CHA NNE (CSEE) NA KIDATO
CHA SITA (ACSEE)
Malengo ya Mitihani wa Kidato cha Nne na Kidato cha Sita ni kupima maarifa, ujuzi na stadi alizopata mtahiniwa za kumwezesha kumudu mahitaji ya sayansi na teknolojia katika kujitegemea, ikiwa ni pamoja na kutimiza mahitaji ya matakwa ya jamii pamoja na mazingira yanayomzunguka. Aidha, matokeo ya mitihani hii huwezesha mamlaka mbalimbali za elimu kuchagua watahiniwa kuendelea na masomo katika ngazi inayofuata ikiwa ni pamoja na elimu ya juu na fani mbalimbali za masomo ya Utalaamu wa Kazi.
Ili kupata maarifa na ujuzi unaotakiwa katika ngazi ya Kidato cha Nne, mtahiniwa wa shule (school candidate) anatakiwa kufanya masomo yasiyopungua saba na yasiyozidi kumi. Kwa upande wa Kidato cha Sita, mtahiniwa anatakiwa kufanya masomo yasiyopungua manne ambayo
miongoni mwake yapo masomo matatu ya tahasusi. Mtahiniwa wa Kujitegemea wa Kidato cha Nne anayefanya mtihani kwa mara ya kwanza anatakiwa kufanya masomo yasiyopungua matatu. Aidha, kwa mtaihiniwa wa kidato cha sita anayefanya mtihani kwa mara ya kwanza anatakiwa
kufanya masomo yasiyopungua mawili likiwemo somo la General Studies.
Ili kupata maarifa na ujuzi unaotakiwa katika ngazi ya Kidato cha Nne, mtahiniwa wa shule (school candidate) anatakiwa kufanya masomo yasiyopungua saba na yasiyozidi kumi. Kwa upande wa Kidato cha Sita, mtahiniwa anatakiwa kufanya masomo yasiyopungua manne ambayo
miongoni mwake yapo masomo matatu ya tahasusi. Mtahiniwa wa Kujitegemea wa Kidato cha Nne anayefanya mtihani kwa mara ya kwanza anatakiwa kufanya masomo yasiyopungua matatu. Aidha, kwa mtaihiniwa wa kidato cha sita anayefanya mtihani kwa mara ya kwanza anatakiwa
kufanya masomo yasiyopungua mawili likiwemo somo la General Studies.
3.0 VIWANGO VYA UFAULU NA UTARATIBU WA KUTUNUKU
3.1 Viwango vya Ufaulu
Katika kutunuku vyeti, Baraza hutumia gredi A, B+, B, C, D, E na F ili
kupambanua ufaulu kwa kila mtahiniwa katika Mitihani ya Kidato cha Nne
na Kidato cha Sita. Mchanganuo wa Viwango vya ufaulu vinavyotumika ni
kama inavyoonekana katika Jedwali la 1.
Jedwali la 1:
kupambanua ufaulu kwa kila mtahiniwa katika Mitihani ya Kidato cha Nne
na Kidato cha Sita. Mchanganuo wa Viwango vya ufaulu vinavyotumika ni
kama inavyoonekana katika Jedwali la 1.
Jedwali la 1:
Viwango vya Ufaulu katika CSEE na ACSEE:
GREDI MFIKO WA MAELEZO
ALAMA
A 75-100 Bora sana (Excellent)
B+ 60-74 Vizuri sana (Very Good)
B 50-59 Vizuri (Good)
C 40-49 Wastani (Average)
D 30-39 Inaridhisha (Satisfactory)
E 20-29 Hairidhishi (Unsatisfactory)
F 0-19 Feli (Fail)
ALAMA
A 75-100 Bora sana (Excellent)
B+ 60-74 Vizuri sana (Very Good)
B 50-59 Vizuri (Good)
C 40-49 Wastani (Average)
D 30-39 Inaridhisha (Satisfactory)
E 20-29 Hairidhishi (Unsatisfactory)
F 0-19 Feli (Fail)
Mtahiniwa atahesabiwa kuwa amefaulu somo endapo atakuwa amepata angalau gredi D (alama 30) katika somo husika. Hivyo, kiwango cha juu cha ufaulu katika somo ni Gredi A ambapo kiwango cha chini cha ufaulu (Pass) katika somo ni Gredi D. Ufaulu katika Gredi A, B+, B na C utakuwa
ni “Credit Pass” kwa CSEE ambapo kwa ACSEE itakuwa ni “Principal Pass”.
3.2 Matumizi ya Alama Endelevu (CA) katika Alama ya Mwisho
Wakati wa kupanga viwango vya ufaulu kama ilivyoainishwa katika Jedwali la 1, uwiano wa alama 30:70 hutumika kukokotoa Alama ya Mwisho (Final Score); ambapo asilimia 30 ni mchango wa Alama Endelevu (CA) na asilimia 70 ni mchango wa Alama za Mtihani wa Taifa (FE). Katika Mtihani wa Kidato cha Nne 2013 na Kidato cha Sita 2014 mchanganuo wa alama 30 za CA ni kama inavyoonekana katika Jedwali la 2 na 3.
Jedwali la 2: Mchanganuo wa CA katika CSEE
Na. Aina ya Mtihani Alama
1 Mtihani wa Taifa Kidato cha Pili 15
2 Matokeo ya Mtihani wa Kidato
cha Tatu – Muhula I
3 Matokeo ya Mtihani wa Kidato 10
cha Tatu – Muhula II
4 Matokeo ya Mtihani wa Kidato
_ cha Nne – Muhula I
5 Kazi Mradi / Project 5
Jumla 30
2 Matokeo ya Mtihani wa Kidato
cha Tatu – Muhula I
3 Matokeo ya Mtihani wa Kidato 10
cha Tatu – Muhula II
4 Matokeo ya Mtihani wa Kidato
_ cha Nne – Muhula I
5 Kazi Mradi / Project 5
Jumla 30
Jedwali la. 3: Mchanganuo wa CA katika ACSEE
- Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Tano Muhula wa I na II itachangia alama 15
- Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita Muhula wa I itachangia alama 10
- Kazi Mradi / Project itachangia alama 5
Hata hivyo, kuanzia Mtihani wa Kidato cha Nne 2014 na Kidato cha Sita 2015, mchango wa CA wa alama 30 utapatikana kutokana na mitihani mbalimbali kama ilivyoaninishwa katika Jedwali la 4 na 5.
Jedwali la. 4: Mchanganuo wa CA katika CSEE
- Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Pili itachangia alama 10
- Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Tatu – Muhula I na Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Tatu – Muhula II itachangia alama 15
- Matokeo ya Mtihani Mock wa Kidato cha Nne itachangia alama 10
- Kazi Mradi / Project itachangia alama 5
Jumla 30
Jedwali la 5: Mchanganuo wa CA katika ACSEE
- Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Tano Muhula wa I na II itachangia alama 15
- Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita Muhula wa I itachangia alama 10
- Kazi Mradi / Project itachangia alama 5
Muhimu: Katika somo ambalo mtahiniwa hakufanyia Kazi Mradi, alama za matokeo ya Mitihani ya Mock ya Kidato cha Nne na Kidato cha Sita itachangia alama 15 badala ya 10 zilizoainishwa katika Jedwali la 4 na 5..
3.3 Utaratibu wa Kutunuku Alama ya Mwisho (Final Score)
Ili kupata Alama ya Mwisho (Final Score), Baraza la Mitihani hukokotoa Alama ya Mwisho kwa kutumia kanuni ifuatayo:
CFM - Alama ya Mwisho ya Mtahiniwa
∂1 - Uwiano wa Alama katika FE
∂2 - Uwiano wa Alama katika CA
FEcm - Alama ya Mtahiniwa katika FE (Candidate’s Mark)
CAcm - Alama ya Mtahiniwa katika CA (Candidate’s Mark)
Mfano: Iwapo katika somo la Geography mtahiniwa amepata alama 13 katika Mtihani wa Mwisho (Final Examination-FE) na Alama Endelevu zilizooneshwa katika Jedwali lifuatalo:
Kidato cha II alipata alama 89
Mitihani ya Darasani:
Ukokotoaji wa alama ya mwisho ya mtahiniwa huyu hufanywa kama ifuatavyo:
(a) Mchango wa Mtihani wa Kidato cha Pili katika CA ni:
(15/30) x 89= 45.5
(b) Mchango wa Mitihani ya Kidato cha Tatu na Kidato cha Nne katika CA ni
(i) Wastani wa alama za Kidato cha Tatu na Kidato cha Nne ni
(92 +93+95)/3 = 93.3
(ii) Hivyo, mchango wa CA katika Kidato cha Tatu na Kidato cha
Nne ni
(10/30)x93.3 = 31.1
(c) Mchango wa alama za Kazi-Mradi utakuwa ni
5/30x68 = 11.3
Hivyo jumla ya alama za CA
45.5 + 31.1 + 11.3= 87.9
Kwa kutumia Kanuni CFM = ∂1*FEcm + ∂2*CAcm na uwiano wa 30:70 CFM = ∂1*FEcm + ∂2*CAcm
Ambapo;CFM - Alama ya Mwisho ya Mtahiniwa
∂1 - Uwiano wa Alama katika FE
∂2 - Uwiano wa Alama katika CA
FEcm - Alama ya Mtahiniwa katika FE (Candidate’s Mark)
CAcm - Alama ya Mtahiniwa katika CA (Candidate’s Mark)
Mfano: Iwapo katika somo la Geography mtahiniwa amepata alama 13 katika Mtihani wa Mwisho (Final Examination-FE) na Alama Endelevu zilizooneshwa katika Jedwali lifuatalo:
Kidato cha II alipata alama 89
Mitihani ya Darasani:
- Kidato cha III Muhulawa 1 alipata 92
- Kidato cha III Muhula wa 2 alipata 93
- Kidato cha IV Muhula wa 1 alipata 95
- Kazi ya miradi alipata 68
Ukokotoaji wa alama ya mwisho ya mtahiniwa huyu hufanywa kama ifuatavyo:
(a) Mchango wa Mtihani wa Kidato cha Pili katika CA ni:
(15/30) x 89= 45.5
(b) Mchango wa Mitihani ya Kidato cha Tatu na Kidato cha Nne katika CA ni
(i) Wastani wa alama za Kidato cha Tatu na Kidato cha Nne ni
(92 +93+95)/3 = 93.3
(ii) Hivyo, mchango wa CA katika Kidato cha Tatu na Kidato cha
Nne ni
(10/30)x93.3 = 31.1
(c) Mchango wa alama za Kazi-Mradi utakuwa ni
5/30x68 = 11.3
Hivyo jumla ya alama za CA
45.5 + 31.1 + 11.3= 87.9
Alama ya Mwisho (CFM) ya mtahiniwa huyu ni
CFM = 70/100x13 + 30/100x87.9 ambayo itakuwa ni 35.
Kwa Alama 35, mtahiniwa huyu atatunukiwa gredi D ya ufaulu katika somo la
Geography.
3.4 Madaraja ya Ufaulu
Baraza la Mitihani la Tanzania hupanga ufaulu katika madaraja mbalimbali. Madaraja hayo hupangwa kwa kutumia mfumo wa Pointi au mfumo wa Grade Point Average (GPA). Katika mfumo wa Pointi, mtahiniwa wa Kidato cha Nne hukokotolewa idadi ya pointi zake alizopata katika masomo saba aliyofanya vizuri na mtahiniwa wa Kidato cha Sita hukokotolewa idadi ya pointi katika masomo matatu ya tahasusi (combination) aliyojisajili. Katika mfumo wa GPA, jumla ya pointi alizopata mtahiniwa wa Kidato cha Nne katika masomo saba aliyofanya vizuri hugawanywa kwa saba Ili kupata wastani wa pointi alizopata mtahiniwa.
Aidha, kwa watahiniwa wa ACSEE idadi ya pointi walizopata katika masomo ya tahasusi hugawanywa kwa tatu ili kupata wastani wa pointi alizopata mtahiniwa katika masomo hayo.
Aidha, kwa watahiniwa wa ACSEE idadi ya pointi walizopata katika masomo ya tahasusi hugawanywa kwa tatu ili kupata wastani wa pointi alizopata mtahiniwa katika masomo hayo.
3.4.1 Madaraja katika Mfumo wa Pointi
Madaraja katika mfumo wa pointi hupangwa kuanzia daraja la kwanza hadi la nne yaani ‘Division One’, ‘Division Two’, ‘Division Three’ na ‘Division Four’ . Aidha, daraja la I-III hubainishwa kwa idadi ya pointi alizopata mtahiniwa wakati daraja la nne hubainishwa kwa kutumia kigezo cha mtahiniwa kufaulu angalau D mbili au angalau C moja au zaidi.
Mchanganuo wa madaraja ni kama ilivyoainishwa katika Jedwali la 6.
Jedwali la 6: Muundo wa Madaraja kwa Kutumia Pointi (CSEE)
DARAJA POINTI/VIGEZO POINTI/VIGEZO
CSEE ACSEE
I 7-17 3-7
II 18-24 8-9
III 25-31 10-13
IV Awe na angalau D Awe angalau na D
mbili au Credit Pass mbili au Principal pass
moja isiyopungua C. moja isiyopungua C
O Aliyepata ufaulu Aliyepata ufaulu
chini ya D mbili chini ya D mbili
Ambapo pointi kwa kila gredi ni kama ifuatavyo:
A = 1, B+ = 2, B = 3, C= 4, D = 5, E = 6 na F = 7
Mfano:
a) Kwa mtahiniwa wa CSEE aliyepata matokeo yaliyoainishwa hapa chini atakuwa na idadi ya pointi katika masomo saba aliyofaulu vizuri zaidi kama ilivyooneshwa katika Jedwali lifuatalo:
Mchanganuo wa madaraja ni kama ilivyoainishwa katika Jedwali la 6.
Jedwali la 6: Muundo wa Madaraja kwa Kutumia Pointi (CSEE)
DARAJA POINTI/VIGEZO POINTI/VIGEZO
CSEE ACSEE
I 7-17 3-7
II 18-24 8-9
III 25-31 10-13
IV Awe na angalau D Awe angalau na D
mbili au Credit Pass mbili au Principal pass
moja isiyopungua C. moja isiyopungua C
O Aliyepata ufaulu Aliyepata ufaulu
chini ya D mbili chini ya D mbili
Ambapo pointi kwa kila gredi ni kama ifuatavyo:
A = 1, B+ = 2, B = 3, C= 4, D = 5, E = 6 na F = 7
Mfano:
a) Kwa mtahiniwa wa CSEE aliyepata matokeo yaliyoainishwa hapa chini atakuwa na idadi ya pointi katika masomo saba aliyofaulu vizuri zaidi kama ilivyooneshwa katika Jedwali lifuatalo:
SOMO Civ. Hist. Geog. Kisw. English Phy. Chem. Biol. Maths
Pointi GRADE A B+ B+ B C C C C E
UZITO WAGREDI 1 2 2 3 4 4 4 4 6
Idadi ya Pointi alizopata katika masomo Saba aliyofanya vizuri zaidi ni
1 + 2+ 2 + 3 + 4+ 4 + 4 = = 20
Hivyo, kwa Pointi 20, mtahiniwa anatunukiwa matokeo
yenye Division Two.
b) Kwa mtahiniwa wa ACSEE aliyepata matokeo yaliyoainishwa
hapa chini atakuwa na idadi ya pointi katika masomo ya tahasusi
kama ilivyooneshwa katika Jedwali lifuatalo:
MASOMO Tahasusi (combination) Ziada
Phy. Chem. Biol. BAM GS
GRADE E B+ A D A
UZITO WA GREDI 6 2 1 5 1
Idadi ya Pointi alizopata katika masomo ya tahasusi
(combination subjects) ni 6 + 2+ 1 = 9.
3.4.2 Madaraja katika Mfumo wa GPA
‘Grade Point Average’ (GPA) ni Mfumo wa Kutunuku ambao huonesha wastani wa pointi alizopata mtahiniwa katika masomo aliyofaulu katika mtihani wake. Madaraja katika mfumo wa GPA hupangwa katika utaratibu wa Distinction, Merit, Credit na Pass ambapo daraja la Distinction ni la ufaulu wa juu zaidi na daraja la Pass ni la ufaulu wa chini. Mtahiniwa hutunukiwa Gredi A, B+, B, C, D, E au F kutegemeana na ufaulu wake katika somo ambapo uzito wa alama katika gredi A = 5, B+= 4, B = 3,C=2, D = 1, E = 0.5 na F = 0. Mtahiniwa atahesabiwa kuwa amefaulu somo endapo atapata Gredi D ambayo ni sawa na uzito wa Pointi 1.
Ukokotoaji wa jumla ya GPA ya mtahiniwa hufanyika kwa kuzingatia masomo ambayo mtahiniwa amefaulu angalau kwa Gredi D na kuendelea (D, C, B, B+ na A). GPA anayopata mtahiniwa hutokana na wastani wa pointi alizopata katika masomo saba aliyofanya vizuri zaidi kwa Mtihani wa Kidato cha Nne au masomo matatu ya tahasusi kwa Mtihani wa Kidato cha Sita. Aidha, GPA ya mtahiniwa huandikwa katika nafasi moja ya Desimali ambapo nafasi ya pili ya desimali hukadiriwa katika makumi yaliyokaribu.
Ukokotoaji wa jumla ya GPA ya mtahiniwa hufanyika kwa kuzingatia masomo ambayo mtahiniwa amefaulu angalau kwa Gredi D na kuendelea (D, C, B, B+ na A). GPA anayopata mtahiniwa hutokana na wastani wa pointi alizopata katika masomo saba aliyofanya vizuri zaidi kwa Mtihani wa Kidato cha Nne au masomo matatu ya tahasusi kwa Mtihani wa Kidato cha Sita. Aidha, GPA ya mtahiniwa huandikwa katika nafasi moja ya Desimali ambapo nafasi ya pili ya desimali hukadiriwa katika makumi yaliyokaribu.
Mfano, mtahiniwa mwenye GPA ya 3.15 itakuwa sawa na 3.2 na mtahiniwa mwenye GPA ya 3.14 itakuwa sawa na 3.1.
Muundo wa madaraja kwa kutumia GPA katika Mitihani ya Kidato cha Nne na cha Sita ni kama ilivyoainishwa katika Jedwali la 7.
Jedwali la 7: Muundo wa Madaraja kwa Kutumia GPA
DARAJA CSEE ACSEE
Distinction 3.6-5.0 3.7-5.0
Merit 2.6-3.5 3.0-3.6
Credit 1.6-2.5 1.7-2.9
Pass 0.3-1.5 0.7-1.6
Fail 0.0-0.2 0.0-0.6
Muundo wa madaraja kwa kutumia GPA katika Mitihani ya Kidato cha Nne na cha Sita ni kama ilivyoainishwa katika Jedwali la 7.
Jedwali la 7: Muundo wa Madaraja kwa Kutumia GPA
DARAJA CSEE ACSEE
Distinction 3.6-5.0 3.7-5.0
Merit 2.6-3.5 3.0-3.6
Credit 1.6-2.5 1.7-2.9
Pass 0.3-1.5 0.7-1.6
Fail 0.0-0.2 0.0-0.6
3.4.3 Kanuni ya Ukokotaoji wa GPA
(a) Kanuni inayotumika kukokotoa GPA ya mtahiniwa katika Mtihani
wa Kidato cha Nne ni
Ambapo
p = pointi za masomo saba ambayo mtahiniwa kafaulu
vizuri zaidi
n = idadi ya masomo saba ambayo mtahiniwa amefanya
vizuri zaidi.
Mfano, Ukokotoaji wa GPA kwa mtahiniwa wa CSEE aliyepata
matokeo yaliyoainishwa hapa chini ni kama ifuatavyo:
SOMO Civ. Hist. Geog. Kisw. English Phy. Chem. Biol. Maths
GRADE A B+ B+ B C C C C E
UZITO WAGREDI 5 4 4 3 2 2 2 2 0.5
(i) Masomo saba ambayo mtahiniwa amefaulu vizuri ni
Civics (A), History (B+), Geograpghy (B+), Kiswahili(B), English (C), Physics (C) na Chemistry (C) ambayo yana uzito wa alama 5, 4, 4, 3, 2, 2 na 2.
(ii) Wastani wa pointi (GPA) alizopata mtahiniwa katika
masomo saba aliyofaulu vizuri ni
(5 + 4 + 4 + 3 + 2 +2 + 2)/7 ambayo itakuwa 3.1.
Hivyo, kwa GPA ya 3.1,mtahiniwa huyu hutunukiwa matokeo yenye Daraja laMerit.
(iii) Mtahiniwa aliyefanya masomo pungufu ya 07, ufaulu wake hautakokotolewa kwa kutumia GPA na badala yake atafaulu katika kiwango cha “Pass” endapo atapata angalau Gredi D mbili au C moja.
(b) Kanuni inayotumika kukokotoa GPA ya mtahiniwa katika Mtihani wa
Kidato cha Sita ni
p= pointi za masomo ya tahasusi (combination subjects)
n = idadi ya masomo ya tahasusi (combination subjects)
Mfano, Ukokotoaji wa GPA kwa mtahiniwa wa ACSEE aliyepata
matokeo yaliyoainishwa hapa chini ni kama ifuatavyo:
MASOMO Tahasusi (combination) Ziada
Phy. Chem. Biol. BAM GS
GRADE E B+ A D A
UZITO WA GREDI 0.5 4 5 1 5
(i) Katika masomo matatu ya tahasusi (combination subjects) ambayo mtahiniwa ameyafanya amefaulu katika masomo mawili ambayo ni Biology (A) na Chemistry (B+) yenye uzito wa alama 5 na 4.
Mtahiniwa amepata Gredi E katika somo la Physics ambalo halitajumuishwa katika GPA kwa kuwa hakulifaulu.
(ii) Wastani wa pointi (GPA) alizopata mtahiniwa utakuwa ni (5 + 4)/3 ambayo ni 3.0. Hivyo, kwa GPA ya 3.0, mtahiniwa huyu hutunukiwa matokeo yenye Daraja la Merit.
(iii) Mtahiniwa aliyefanya masomo pungufu ya 03, ufaulu wake hautakokotolewa kwa kutumia GPA na badala yake atafaulu katika kiwango cha “Pass” endapo atapata angalau Gredi D mbili au C moja.
wa Kidato cha Nne ni
GPA= (∑p)/n
Ambapo
p = pointi za masomo saba ambayo mtahiniwa kafaulu
vizuri zaidi
n = idadi ya masomo saba ambayo mtahiniwa amefanya
vizuri zaidi.
Mfano, Ukokotoaji wa GPA kwa mtahiniwa wa CSEE aliyepata
matokeo yaliyoainishwa hapa chini ni kama ifuatavyo:
SOMO Civ. Hist. Geog. Kisw. English Phy. Chem. Biol. Maths
GRADE A B+ B+ B C C C C E
UZITO WAGREDI 5 4 4 3 2 2 2 2 0.5
(i) Masomo saba ambayo mtahiniwa amefaulu vizuri ni
Civics (A), History (B+), Geograpghy (B+), Kiswahili(B), English (C), Physics (C) na Chemistry (C) ambayo yana uzito wa alama 5, 4, 4, 3, 2, 2 na 2.
(ii) Wastani wa pointi (GPA) alizopata mtahiniwa katika
masomo saba aliyofaulu vizuri ni
(5 + 4 + 4 + 3 + 2 +2 + 2)/7 ambayo itakuwa 3.1.
Hivyo, kwa GPA ya 3.1,mtahiniwa huyu hutunukiwa matokeo yenye Daraja laMerit.
(iii) Mtahiniwa aliyefanya masomo pungufu ya 07, ufaulu wake hautakokotolewa kwa kutumia GPA na badala yake atafaulu katika kiwango cha “Pass” endapo atapata angalau Gredi D mbili au C moja.
(b) Kanuni inayotumika kukokotoa GPA ya mtahiniwa katika Mtihani wa
Kidato cha Sita ni
GPA= (∑p)/n
Ambapo p= pointi za masomo ya tahasusi (combination subjects)
n = idadi ya masomo ya tahasusi (combination subjects)
Mfano, Ukokotoaji wa GPA kwa mtahiniwa wa ACSEE aliyepata
matokeo yaliyoainishwa hapa chini ni kama ifuatavyo:
MASOMO Tahasusi (combination) Ziada
Phy. Chem. Biol. BAM GS
GRADE E B+ A D A
UZITO WA GREDI 0.5 4 5 1 5
(i) Katika masomo matatu ya tahasusi (combination subjects) ambayo mtahiniwa ameyafanya amefaulu katika masomo mawili ambayo ni Biology (A) na Chemistry (B+) yenye uzito wa alama 5 na 4.
Mtahiniwa amepata Gredi E katika somo la Physics ambalo halitajumuishwa katika GPA kwa kuwa hakulifaulu.
(ii) Wastani wa pointi (GPA) alizopata mtahiniwa utakuwa ni (5 + 4)/3 ambayo ni 3.0. Hivyo, kwa GPA ya 3.0, mtahiniwa huyu hutunukiwa matokeo yenye Daraja la Merit.
(iii) Mtahiniwa aliyefanya masomo pungufu ya 03, ufaulu wake hautakokotolewa kwa kutumia GPA na badala yake atafaulu katika kiwango cha “Pass” endapo atapata angalau Gredi D mbili au C moja.
4.0 HITIMISHO
Baraza la Mitihani limeandaa Mwongozo huu ili kuwawezesha wadau kujua viwango vya ufaulu vinavyotumika pamoja na utaratibu wa matumizi ya Alama Endelevu (CA) katika kutunuku matokeo ya Mitihani ya Kidato cha Nne (CSEE) na Kidato cha Sita (ACSEE).
Baraza la Mitihani la Tanzania linaamini kuwa Mwongozo huu utakuwa ni chachu kwa Wadau wa Elimu hususan Walimu na Wanafunzi ya kuongeza bidii katika ufundishaji na ujifunzaji ili kufikia viwango vya juu vya ufaulu vilivyoainishwa.
Baraza la Mitihani la Tanzania linaamini kuwa Mwongozo huu utakuwa ni chachu kwa Wadau wa Elimu hususan Walimu na Wanafunzi ya kuongeza bidii katika ufundishaji na ujifunzaji ili kufikia viwango vya juu vya ufaulu vilivyoainishwa.
IMETOLEWANA:
BARAZALAMITIHANI LA TANZANIA
S.L.P 2624
DAR ES SALAAM
APRILI, 2014
0 comments:
Post a Comment