Tuesday, 19 August 2014

Kwa Waliokosa Nafas ya Kujiandikisha kwenye vitambulisho vya taifa

                              www.nida.go.tz


Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) inapenda kuwajulisha wakazi wa mkoa wa Dar es Salaam wenye umri wa miaka 18 na zaidi ambao hawakupata fursa ya kujiandikisha au kuchukuliwa alama za vidole na picha kufika kwenye ofisi za NIDA za wilaya kupata huduma hizi. Ofisi hizi katika kila wilaya ni:-
WILAYA YA ILALA
1.    Tabata Shule
2.    Gongo la Mboto (Kituo Kipya)

WILAYA YA TEMEKE
1.    Chang’ombe bango lipo kituo cha Bora karibu na ofisi za TRA
2.    Kigamboni karibu na Msikiti wa Aziza.

WILAYA YA KINONDONI
1.    Goig – Mbezi Beach mkabala na Shamo au jengo la Maktech
2.    Magomeni jengo la TTCL karibu na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Kinondoni.


Siku za kutoa huduma: Jumatatu – Jumamosi Saa 02:00 Asubuhi – Saa 09:30 Alasiri.
Imetolewa na;
Mkurugenzi Mkuu
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA)

Share:

0 comments:

Post a Comment