Thursday, 21 August 2014

Mhe. Mwigulu Nchemba atoa wito kwa Sekta binafsi kuchangamkia fursa

Lorietha Laurence
Naibu  Waziri  wa Fedha Mhe.Mwigulu  Nchemba  ametoa wito kwa sekta binafsi kutumia fursa zinazotolewa nchini ili kujifunza  aina ya miradi inayoweza kukopesheka.
Hayo yamezungumzwa leo jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa semina ya wafanyabiasahara iliyoandaliwa na Benki ya Maendeleo ya Wafanyabiashara Mashariki na Kusini mwa  Afrika (PTA).
Aliongeza  kusema kuwa Tanzania ni nchi yenye fursa nyingi na kwa kupitia semina  hii itasaidia katika  kukabiliana na changamoto mbalimbali za kimaisha kutokana na mafunzo yanayotolewa.
Naye Rais Mtendaji  Mkuu wa Benki ya PTA bw.Admassu Tadesse amefurahishwa na muitikio wa watanzania katika kuhudhuria semina hiyo na utayari wao kutaka kujifunza mbinu mbalimbali za kibiashara .
“Najisikia furaha kuwepo mahali hapa  kuweza kushirikiana nanyi katika semina hii kwani najifunza mengi kutoka kwenu kama ambavyo nanyi mnavyojifunza kutoka kwetu na huu ni ushirikiano mzuri wenye kuleta maendeleo “ alisema  Tadessa.
Benki ya PTA  inatoa huduma zake kwa  nchi wanachama ikiwa na lengo la kuwa Taasisi ya kifedha inayoongoza  Mashariki na Kusini mwa Afrika katika utoaji wa huduma za kibenki ambapo
mwaka huu imetimiza miaka 30 tangu kuanzishwa kwake mnamo mwaka 1985.
Share:

0 comments:

Post a Comment