Saturday 25 April 2015

Majukumu Ya Meya/Mwenyekiti wa Halmashauri,Madiwani,Viongozi wa Vijiji,Mitaa na Vitongoji.

Image result for TANZANIA EMBLEM

Imetolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
 
1.0 UTANGULIZI
Kwa mujibu wa ibara ya 145 na 146 Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali za Mitaa ni vyombo vya haki na vyenye mamlaka ya kushiriki na kushirikisha wananchi katika kupanga na kutekeleza shughuli za maendeleo na utoaji wa huduma katika sehemu zao. Serikali za Mitaa huanzishwa kwa madhumuni ya kuwahudumia wananchi na kuwapelekea madaraka kwa kuwajengea uwezo wa kiuchumi, kijamii, kisiasa na kiutamaduni.
Sifa muhimu zinazozitambulisha Serikali za Mitaa ni pamoja na:
  1. Kuundwa kwa mujibu wa Katiba na Sheria.
  2. Ni vyombo vya wananchi ambavyo huundwa, huendeshwa, husimamiwa na kuwajibika kwa wananchi.
  3. Hujenga demokrasia kuanzia ngazi ya msingi.
  4. Huleta maendeleo ya wananchi kwani ziko karibu nao.
  5. Ni vyombo vya uwakilishi wa wananchi katika Serikali
Tafadhali bofya hapa chini Kwa Ufaanuzi wa kina.
Share:

0 comments:

Post a Comment