SOMO LA PILI : UTENGENEZAJI WA MISHUMAA.
![]() |
Mishumaa., Utengenezaji wa mishumaa huweza kusaidia kuongeza kipato cha mjasiriamali, kwani bidhaa hii huitajika sana kwa matumizi mbalimbali kama vile matumizi ya majumbani nakadhalika. |
1. Paraffin Wax
2. Utambi
3. Mould ( Umbo )
4. Stearine au mixture
5. Rangi
6. Jiko la mafuta ya taa au mkaa.
7. Sufuria.
8. Boric acid.
![]() | ||||||
Paraffin Wax. |
VIDOKEZO MUHIMU :
1. Paraffin Wax :
Hii inatokana na nta na sega ya nyuki iliyo changanywa na mafuta ya taa. Ina rangi nyeupe na katika utengenezaji wa mishumaa ina ubora kuliko bee wax.
* Bee Wax : Inatokana na masega ya nyuki yaliyo changanywa na mafuta ya petroli na diesel na rangi yake ni ya njano.
2. STEARINE
Hii dawa maalumu inayo fanya mishumaa iungane ama ishikamane.
![]() |
Mould ( Umbo ) . Mfano wa umbo linalo weza kutumika kutengeneza mishumaa. Hata hivyo, unaweza kutengeneza umbo lolote kwa kadri unavyo taka " shape " ya mishumaa yako iwe. |
4. RANGI : Rangi nzuri zinazo tumika katika utengenezaji mishumaa ni rangi za chakula na nyingi huwa ni za maji.
![]() |
Boric acid , hii ni maalumu kwa ajili ya kuufanya utambi usiishe mapema na kuufanya uwake bila kutoa moshi. |
JINSI YA KUTENGENEZA
Andaa mould ( umbo lako ) utakalo litumia baada ya kuyeyusha ( paraffin wax ) na kuchanganya na michanganyo yote.
Kwa Mfano : ( Kipimo cha stearine )
1. Wax kilo moja - Stearine vijiko vinne vya chakula.
2. Wax nusu kilo - Stearine vijiko vinne vya chakula
3. Wax robo kilo - Stearine kijiko cha chakula.
Source: Rafiki Elimu Foundation
0 comments:
Post a Comment