Wednesday 3 September 2014

ELIMU YA UJASIRIAMALI: UTENGENEZAJI WA WINE YA NDIZI

SOMO LA SABA : UTENGENEZAJI WA WINE YA NDIZI

Wine  ya  Ndizi.
 Wine  ya  ndizi  inatokana  na  ndizi  mbivu.  Aina  yoyote  ya  ndizi  ambayo  inaweza  kuwiva  inaweza  kutumika  kutengeneza  wine.

Ili  wine  yako  iweze  kuwa  na  kilevi  ni  lazima  uichanganye  na  amira, usipoweka  amira  wine  yako  itakuwa  tamu  lakini  isiyokuwa  na  kilevi.

MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  WINE  YA  NDIZI.

*  Ndizi   zilizo  iva  vizuri.

* Maji

*  Vyombo  vya  kuhifadhia.

*  Amira

* Sukari.


HATUA  ZA  KUFUATA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  WINE  YA  NDIZI.

                                              HATUA  YA  KWANZA :

*  Chukua   ndizi  kg.3  zilizo  menywa  maganda  na  ambazo  zimeiva  vizuri, katakata   vipande  vidogo  na  weka  katika  chombo  ambacho  utatumia  kuchachulia  wine  yako.


*  Baada  ya  kupata  hivyo  vipande  vidogo  vidogo , vichanganye  kwenye  maji  lita  ( 5 )  na   baada  ya  hapo  chemsha   kwa  muda  wa  dakika  30.

* Acha  mchanganyiko  wako  huo  upoe.

                                                    HATUA   YA  PILI

*  Changanya  mchanganyiko  wa  ndizi  na  sukari  kikombe  kimoja   cha  chai, koroga  kisha  changanya  na  amira   vijiko  vinne (  4  )  vya  sukari, koroga  tena.

*  Acha  kwa  muda  wa  siku  nne,   siku  ya  nne  utakapo  kwenda  kuitazama  wine  yako  utakuta  povu, hii  ina  maana  kuwa  wine  yako  itakuwa  imeanza  kuchachuka   vizuri.

*  Siku  ya  tano  (  5  )  chuja  wine  yako  vizuri  kwa  kutumia  kitambaa  lakini  bila  kufinyanga, iache  wine  imwagike  yenyewe.

                                               HATUA  YA  TATU 

* Iweke   wine  yako  kwenye  chombo  cha  kutolea  hewa  na   kupunguza  gas  kwa  siku  1  mpaka  miezi  3.

*  Baada  ya  siku  21  wine  yako  itakuwa  tayari.
Share:

0 comments:

Post a Comment